Nilipokuwa na umri wa miaka 16, sikupendezwa hata kidogo na uzito wangu. Sijawahi kuwa mnene kupita kiasi. Mimi ni mnene kiasi tu. Nilijiambia kwamba ikiwa ningekuwa mwembamba, vijana wangenipenda. Kwa hiyo nilijinyima chakula ili niwe na mwili wenye kupendeza.
Nilifaulu kuwa mwembamba lakini pia nikajiletea matatizo ya afya. Ingawa matatizo hayo yalishughulikiwa, bado madhara ya kihisia niliyopata hayajaondoka.
Hadi leo, siwezi kula vizuri. Kadiri muda umepita, ndivyo nimeanza kukubali sura yangu. Mimi hula vizuri na kufanya mazoezi. Lakini ninaposhuka moyo kwa sababu ya jambo nililofanya, mara moja mimi hujiadhibu kwa kukataa kula.
Ikiwa ningeweza, ningewaambia vijana wengine wakumbuke kwamba kila mtu ana maoni yake. Haidhuru una sura ya aina gani, sikuzote kutakuwa na watu wanaoona kuwa unavutia na wengine walio na maoni tofauti.
Jambo muhimu ni kwamba wewe una afya nzuri. Hilo ndilo jambo la maana kwa wale ambao kwa kweli wanakujali.
0 comments: