Siri ya Kufanikiwa: Usikose kula hata mlo mmoja! Ukikosa, utahisi njaa na
huenda ukashawishika kula chakula kingi.
Bila shaka watu fulani ambao
hujiambia “Ninahitaji kupunguza uzito wangu” wana maoni yasiyofaa kuhusu mwili
wao. Kwa kweli hawana tatizo lolote la kunenepa kupita kiasi. Hata hivyo, vipi
ikiwa unahitaji kupunguza uzito? Ona jinsi msichana anayeitwa Catherine alivyofanikiwa.