Mwanaume
anamuhitaji mwanamke zaidi kama msaidizi wake kuliko mwanamke anavyomhitaji
mwanaume na sema hivyo sio kwa kuegemea swala la ngono bali kwenye maswala
mengine mengi ya kimaisha.
Inasemekana kwamba wanawake ambao hawajaolewa wanaishi zaidi ukilinganisha na
wale walio ndani ya ndoa na Wanaume waliondani ya ndoa huishi maisha marefu
zaidi kuliko wale walio nje ya ndoa, umewahi kujiuliza kwanini wataalamu
wanadai hivo?
Kuishi muda mrefu bila
kuwa na kazi kuna madhara mengi kisaikolojia, watu wengi hupatwa na vichaa na
wengine, kujiingiza katika ulevi wa kupindukia, utumiaji dawa za kulevya na
uhuni kutokana na kukata tamaa ya maisha hasa wanapopoteza kazi au wanapomaliza
masomo na kukosa ajira walizokuwa wakizitazamia.
Hii
inatokana na watu wengi kukosa elimu ya namna ya wanavyoweza kutumia vizuri
muda wao wa dhahabu wanapokuwa hawana kazi. Unaitwa muda wa dhahabu au
‘Unemployment golden time’ kwa sababu mkosa ajira huathirika endapo atashindwa
kutumia muda wa awali kujiokoa na makucha ya kukosa kazi.
Ni mara ngapi unawaza kuhusu “KESHO” je umeshawahi
kujiuliza jinsi inavyozuia mafanikio yako kimaisha? Uchunguzi unaonesha kwamba
watu wengi ambao hawajafanikiwa mpaka sasa kwenye maisha yao ni wale
wanaofikiria zaidi kesho na kupuuza leo.
Katika hali ya kawaida mafanikio ya kesho hayapo, yakiwepo ujue yametokana na
leo. Kama utakuwa mtu wa kusema moyoni mwako nitakwenda kazini kesho,
nitajituma zaidi kesho, nitafanya hiki na kile kesho utajikuta kesho haziishi
na kila zikujiapo huja tupu.
Kama
ilivyo mambo mengine kuwa “affection” ni swala la kujifunza, baadhi ya wanaume
waliokuzwa/kulia kwenye jamii yenye mfumo Dume (Waafrika kwa ujumla) huwa
hawajui kuonyesha hilo hitaji, ebu tuliite “kupenda kwa vitendo” hivyo huenda
sio kwamba hataki bali hajui.
Kwa maana hiyo sio mbaya ikiwa wewe mwanadada ukamfundisha nini cha kufanya,
ikiwa na wewe ulikuwa hujui basi jifunzeni wote ili kuwa na uhusiano bora wenye
furaha.
Watu wengi husindwa
kubana matumizi kutokana na kukosa elimu ya jinsi ya kutumia pesa. Baadhi
wamesoma na wengine wanaendelea kusoma masomo mbalimbali yanayohusu pesa na
wanahitimu vizuri, lakini wanapokuja katika uhalisia wa maisha wanajikuta
wanafeli vibaya kutokana na kutoutambua umuhimu wa kuwa na nidhamu ya pesa.
Msomaji wangu nikupe dondoo kadhaa ambazo kwa namna moja ama nyingine zinaweza
kukusaidia katika kubana matumizi na hatimaye hata kama kipato chako ni kidogo,
kikakidhi mahitaji yako muhimu na pia kukawepo na ziada.
Dean Ornish, ambaye ni daktari na
pia mwandishi anaandika hivi: “Upendo na mahusiano ya karibu ni sababu kuu
zinazoweza kutufanya tuwe wagonjwa au tuwe wenye afya, tuhuzunike au tuwe wenye
furaha, tuteseke au tupone.